Monday, July 9, 2012

Jamaa aliye mvamia wema apewa kichapo cha mbwa mwizi

Warembo waliolikamata soko la filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper na Wema Sepetu nao walitia fora kwa pambano lao kali la masumbwi. Pambano hilo la raundi tatu ambalo lilitarajiwa kumaliza bifu la siku nyingi kati ya wanyange hao, lilitanguliwa na pambano kati ya Kanda Kabongo na Ramadhan Kido, lililomalizika kwa Kabongo kushinda kwa pointi. Mpaka pambano la Wema na Wolper linamalizika kwa droo, uwanja mzima ulikuwa ukishangilia kwa nguvu.
Katika tukio lingine lililowashangaza wengi, baada ya Wema kumaliza pambano, shabiki mmoja ambaye hakufahamika alikotokea, alimvamia msanii huyo akiwa anateremka ulingoni na kumkumbatia kwa nguvu lakini kabla hajamdhuru msanii huyo, polisi walimdaka juujuu na kumshushia kichapo cha haja kabla ya kutolewa nje mzobemzobe.

No comments:

Post a Comment