Thursday, July 19, 2012

CRISTIANO RONALDO AMFUNIKA LIONEL MESSI KWA UTAJIRI - FLOYD MAYWEATHER ASHIKA NAMBA MOJA LISTI YA WANAMICHEZO WANAOLIPWA FEDHA NYINGI 2012




Bondia wa kimataifa wa Marekani aliyepo jela kwa sasa Floyd Mayweather Jr. ametajwa na jarida la Forbes kuwa ndio mwanamichezo anayeingiza fedha nyingi kwa mwaka, akiwa amepeleka banki dola millioni 85,000,000 katika kipindi cha miezi 12 iliyopita. Mayweather anafuatiwa na mpinzani wake mfilipino Manny Pacquiao aliyeingiza kiasi cha $62 million.
 
Pamoja na mchezo wa soka kuwa ndio maarufu zaidi lakini wacheza soka wenyewe wameshindwa kuingia hata kwenye Top 5, ingawa wapo kwenye 10 bora. Muingereza David Beckham akishika nafasi ya nane kwa kuingiza millioni 46 USD, huku akifuatiwa na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid ambaye amepeleka bank kiasi cha $42 million. Mchezaji bora wa dunia wa soka Lionel Messi hayumo kwenye top 10, japo hayupo mbali akiwa nafasi ya 11 kwa kuingiza kiasi cha $39 million.


No comments:

Post a Comment